Posts

Showing posts from April, 2018

KUELEKEA MTIHANI WA TAIFA MWEZI MEI, WANAFUNZI 1003 KIDATO CHA SITA SIMIYU WAPIGA KAMBI YA KITAALUMA

Na Stella Kalinga Simiyu Takribani wanafunzi 1003 wa Kidato cha sita kutoka shule za Sekondri 11 zenye kidato cha tano na sita Mkoani Simiyu wamepiga kambi katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na Shule ya Sekondari Binza, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mtihani wa Taifa ambao unatarajia kufanyika mapema mwezi Mei mwaka huu. Akifungua kambi hiyo leo  katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa wilayani Maswa, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Anthony Mtaka amesema ili mkoa huo uweze kushindana na kufanya mageuzi katika Uchumi ni lazima kuwekeza katika elimu. “Kama wanafunzi wetu wanakaa makambi ya michezo ngazi ya kata, wilaya, mkoa na Taifa kwa nini wanafunzi hao hao wasikae  kambi kwa ajili ya maendeleo ya taaluma; tukitaka kufanya mageuzi ya Mkoa huu ni lazima tuweke nguvu kwenye elimu, maeneo yenye uchumi mzuri wamewekeza sana kwenye elimu” alisema Mtaka. Aidha, Mtaka awataka wanafunzi wote wa kidato cha sita kuwasikiliza walimu watakaokuwa wakiwafu...

TUUNGE MKONO JUHUDI ZA VIONGOZI WETU TUIJENGE MASWA YETU

Image
      MASWA YETU          Anaandika mothes mbembela Ndugu wapenzi wasomaji wa Makala zangu Napenda kuwaalika tena katika uchambuzi wa makala zangu ambazo mara nyingi zimekuwa zikiegemea katika kujadili masuala mbalimbali kutoka katika wilaya yangu ya Maswa mkoani Simiyu. Leo katika makala hii ningependa kujikita zaidi katika kutabainisha mambo mbalimbali ya kijamii, kiuchumi na kisiasa ambayo kwa kiasi kikubwa yanafanya MASWA YETU ionekane angavu Daima. Katika wilaya yetu Maswa Juhudi mbalimbali zimeweza kufanywa na viongozi kwa kushirikiana na wananchi wao kuhakikisha kuwa wilaya yetu haipo mbali ktk kilele cha maendeleo, kwa ufupi tu niweze kuorodhesha mambo na assets mbalimbali ambazo kwa Hakika Maswa Tunajivunia. 1. Tuna Hospitali kubwa ya wilaya ambayo imekuwa ikihudumia maelfu ya wagonjwa kutoka sehem mbalimbali za nchi yetu tena kwa kiwango cha juu kabisa (Science and Technology) Hongera ya pekee imfikie Dokta...