Posts

Showing posts from December, 2018

KUTOKA UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA MWALIMU JULIUS NYERERE DAR.

Image
YALIYOJIRI WAKATI WA MAPOKEZI YA NDEGE MPYA YA AIRBUS 220-300 KATIKA UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA JULIUS NYERERE LEO TAREHE 23 DESEMBA, 2018 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli #Nawapongeza watanzania kwa kuamua kulipa kodi, tunafanya haya kwa sababu ya kulipa kodi, hongereni sana Watanzania. #Watanzania nawasisitiza tuwe wazalendo, hii ni kwa faida ya taifa letu. #Uchumi wa nchi yetu unaenda vizuri, tutunze amani yetu, tunarasilimali nyingi, Tanzania ni tajiri. #Pamoja na kuleta ndege mpya tunafufua karakana yetu kubwa ya matengenezo ya ndege iliyopo Kilimanjaro. #Tuliahidi kuimarisha huduma za usafiri, na katika miaka hii mitatu tumetekeleza ahadi hii kwa vitendo ikiwa ni kwa kufanya mambo makubwa ardhini, angani na hata majini. #Tunafanya upanuzi na ukarabati wa viwanja vya ndege 11 nchini, lengo ni kuendelea kuboresha sekta ya usafiri  wa anga. #Watendaji wakuu wa Serikali waliolipiwa tiketi za ndege za ATCL na hawakusafiri warudishe fedh...

MWANAMALUNDI, MSUKUMA ALIYEMSHINDA MKOLONI

Image
Kwa Hisani ya Mwandishi wa  kitabu chake NG'WANAMALUNDI SHUJAA WA WAKISUKUMA ALIYEWATESA WAJERUMANI. Kwa wale waliopata kusoma historia au kusikia hadithi za makabila, hasa ya Wasukuma na Wanyamwezi, hawakukosa kusikia habari ya Ng’wanamalundi. Mtu huyo aliyewahi kuutingisha utawala wa Wajerumani, alizaliwa katika ukoo wa kawaida akiwa mcheza ngoma mashuhuri, mwaka wa kuzaliwa kwake haufahamiki ila alifariki dunia mwaka 1936, akiwa tayari mtu mzima. Watu wengi wamekuwa wakimjadili kwa maoni tofauti, wengine wakimsifu kama shujaa huku wengine wakihusisha uwezo wake na nguvu za giza. Katika makala hii usahihi wa historia yake unaelezwa na mjukuu wake wa pili, Kishosha Sitta (80) mkazi wa Kijiji cha Mwalugulu wilayani Kahama mkoani Shinyanga, anayesimulia alivyomfahamu babu yake huyo. Sitta anaanza kueleza kuwa jina halisi la babu yake halikuwa Ng’wanamalundi bali lilikuwa Igulu Bugomola, ambaye alizaliwa katika Kijiji cha Mwakubunga Nera wilayani Kwimba mkoani Mwa...