KUTOKA UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA MWALIMU JULIUS NYERERE DAR.

YALIYOJIRI WAKATI WA MAPOKEZI YA NDEGE MPYA YA AIRBUS 220-300 KATIKA UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA JULIUS NYERERE LEO TAREHE 23 DESEMBA, 2018

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli

#Nawapongeza watanzania kwa kuamua kulipa kodi, tunafanya haya kwa sababu ya kulipa kodi, hongereni sana Watanzania.

#Watanzania nawasisitiza tuwe wazalendo, hii ni kwa faida ya taifa letu.

#Uchumi wa nchi yetu unaenda vizuri, tutunze amani yetu, tunarasilimali nyingi, Tanzania ni tajiri.

#Pamoja na kuleta ndege mpya tunafufua karakana yetu kubwa ya matengenezo ya ndege iliyopo Kilimanjaro.

#Tuliahidi kuimarisha huduma za usafiri, na katika miaka hii mitatu tumetekeleza ahadi hii kwa vitendo ikiwa ni kwa kufanya mambo makubwa ardhini, angani na hata majini.

#Tunafanya upanuzi na ukarabati wa viwanja vya ndege 11 nchini, lengo ni kuendelea kuboresha sekta ya usafiri  wa anga.

#Watendaji wakuu wa Serikali waliolipiwa tiketi za ndege za ATCL na hawakusafiri warudishe fedha wenyewe tunataka thamani ya fedha zetu.

#Naamini pia wafanyakazi wa Air Tanzania mtaendelea kuhakikisha mnazalisha faida na kutoa huduma bora maana nimeanza kuona baadhi ya malalamiko.

*Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe*

#Tutafanya kila jitihada za kuhakikisha tunaendelea kuliboresha Shirika letu la ndege.

#Tumeweka mipango ya kufufua karakana yetu ya matengenezo ya ndege iliyopo Kilimanjaro, ndege zetu zitakarabatiwa hapahapa.

*Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi Balozi John Kijazi*

#Ndege hii ni ya tano kuwasili nchini katika kipindi cha miaka mitatu ya Rais Magufuli na Tanzania ni ya kwanza Afrika kununua ndege hii.

#Mwezi January tunategemea kupokea ndege nyingine kama hii.

*Katibu Mkuu Sekta ya Uchukuzi Dkt. Leonard Chamuhiro*

#Leo tunapokea ndege moja kati ya mbili ikiwa ni sehemu ya mpango wa ufufuaji wa Shirika letu la ndege.

#Ndege hizi ni mpya kabisa na za kisasa , Tanzania ndio nchi ya kwanza barani Afrika  kununua ndege hizi na zina uwezo wa kubeba abiria 132.

#Ndege hizi zinauwezo wa kuruka moja kwa moja bila kusimama kwa masaa sita na nusu.

#Idadi ya abiria wanaotumia Shirika leo wameongezeka kutoka 5600 hadi kufikia abiria 34,000 kwa mwezi.

*Mkuu wa Mkoa wa Dar wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda*

#Maendeleo haya yote ni kwasababu watanzania tumeamua kuungana na kulipa kodi, tuendelee kufanya hivi kwa ustawi wa nchi yetu.

Imetolewa na Idara ya Habari- MAELEZO
UVCCM MASWA NGUVU MOJA

Comments

Popular posts from this blog

SIMANZI

ZIARA YA KATIBU MKUU WA CCM MASWA MKOANI SIMIYU YALETA NEEMA UKAMILISHWAJI WA JENGO LA KITEGA UCHUMI LA CCM. NYONGO ASHITUKIZA HARAMBEE