Posts

KHERI YA MWAKA MPYA

Kwaniaba ya Umoja wa vijana wa chama Cha mapinduzi Wilaya ya Maswa, napenda kuwatakia Kheri ya mwaka mpya 2022. Ukawe mwaka wenye Kheri ,neema na Mafanikio makubwa kwa kila mmoja wetu. Masaga John Paul. Mwenyekiti wa UVCCM wilaya ya Maswa (M/k/ siasa)

SAMIA TENA 2025-30

Kwa Niaba ya vijana wote Kanda ya ziwa na  Kati bila ya kujari itikadi zetu za Dini ,siasa, ukanda au vyama vyetu vya siasa. Tunakupongeza kwa kuendeleza vyema taifa letu Tanzania kwa kudumisha Amani, Mshikamano na ustawi wa jamii. Taifa linasonga mbele kisiasa, uchumi na hata kijamii. Hongera Mhe SAMIA SULUHU HASSAN Vijana tunakuelewa zaidi.

TUMEWAKOSEA WAMACHINGA

* Msimamo wangu Binafsi juu ya suala la Machinga * Kwanza nitoe pole kwa ghasia na taharuki na Mabadiriko ya ghafla zidi ya waMachinga Bodaboda, Mama Rishe na woote walioghubikwa na Mambo ya kupangana mjini na huenda vijijini. Kwangu Binafsi naona mmewakosea Sana kundi la jamii hii ya wafanya kazi na haswaa waliojiajiri kupitia umachinga. Na Declare intest kuwa Mimi Ni Machinga. Pia nakubaliana na Mpango mzuri wa serikali kwa tunachokiita Uwepo wa mpango wa maeneo maalum ya biashara za wamachinga na namna Boda boda watakavyokuwa wanaingia na kutoka mjini. Lakini wateule mmekurupupa mno juu ya Jambo hili na mmegharimu maisha yetu na Maisha ya wanchi (siwaiti wanyonge nawaita wajenzi wa taifa na walipa Kodi). Suala hili lilipaswa liwe shirikishi na Mpango wa muda mrefu wa kubainisha maeneo, changamoto  zao  na utaratibu mzuri wa kazi zao za  kichinga na Bodaboda kabla ya kutufurumusha,  sio suala la kukurupushana namna hiii (Chama changu kupitia mwenenezi taifa nakubaliana na kauli ku...

DAKIKA 45 ZA KIPINDI CHA KWANZA KWANU WATEULE

Image
  Ndugu watanzania wenzangu , mabibi na mabwana vijana kwa wazee, nianze kwa kumshukuru Mungu kwa uzima na afya njema kwetu sote lakini nitoe pole kwa wale wote ambao hali zenu sio nzuri kiafya pamoja na mambo mengine, hata hivyo kila lililo kheri nawatakieni. Nianze kwa kumpongeza Dr John Pombe Magufuli Rais wa awamu ya tano wa jamhuri ya muungano wa Tanzania  kwa mara nyingine kwa  kuaminiwa na watanzania wote kuendelea kuwaongoza kwa ushindi wa kishindo wa zaidi ya asilimia 81, wakiwa pamoja na mwana mama hodari kabisa Samia Hassan katika uchaguzi mkuu wa october 2020. lakini kwa kipekee nikipongeze chama cha mapinduzi CCM chini ya uongozi wa dr John Pombe Magufuli kwa kuendelea kuaminika na Umma wa Tanzania  hata hivyo pongezi ziende kwao viongozi wa CCM wa ngazi zote kwa kazi kubwa walizofanya katika kuhakikisha CCM inaendelea kushinda chaguzi ili kuunda serikali. niishukuru serikali ya awamu ya tano kwa kutekeleza vyema na kishindo ilani ya uchaguzi ya mwaka 20...

TUSICHUKULIE POA CORONA INAZUILIKA

Image
Ndugu wadau wanahabari, vijana wenzangu, wasomaji pamoja na wasikilizaji wetu Habari zenu Binafsi. Nianze kwa kuwakumbusha na kuwafahamisha kuwa bado Duniani kote wanahangaika, kuzuia na kupambana na ugonjwa huu wa Corona. hata hapa Tanzania tayari tumekuwa tukipokea Taarifa na hali ya udhihiti wa ugonjwa huu wa Corona hata hivyo Niwaombe muendelee kufuaata maelekezo ya serikali ya namna ya kujikinga pamoja na kuzitekeleza kwa vitendo tahadhari zinazotolewa kupitia wizara ya afya na kamati iliyoundwa na waziri mkuu. Ndugu wadau wa habari  na Wana maswa mnaotumia mitandao kazaa ya kijamii whatsp, Instagram, Facebook na mingineneo zitumieni mitandao hizo kwa kuendele kuelimisha na kuikumbusha jamii na pia kuhamasisha usafi na uchukuaji wa tahadhari zinazotolewa na serikali kwani mitandao ya kijamii imekuwa ni chachu ya kupokea na kutoa Taarifa zinazojili tumieni muda wenu wa kukaa katika Magroup hayo kwa faida na kushusha hamasa hizo kwa familia zetu na jamii zetu zinazotuzunhuka. Ug...

ASANTE RC MTAKA KWA UAMUZI MZURI WA KUSHUSHA BEI KWA WATEJA WASIO NA MITA ZA MAJI

MKUU WA MKOA WA SIMIYU ASHUSHA BEI YA MAJI MASWA. Mkuu wa mkoa wa Simiyu,Antony Mtaka ameiagiza Mamlaka ya Maji na usafi wa Mazingira mjini Maswa(Mauwasa) kushusha bei ya maji kwa wateja wao wasio na dira(Mita)kutoka sh 25600 hadi Sh 17600 kwa mwezi. Uamuzi huo ameutoa leo ktk viwanja vya Madeco mjini Maswa alipofanya mkutano wa hadhara wa kusikiliza malalamiko ya wananchi juu ya kupanda bei hizo kutoka Sh 5600 hadi Sh 25,600 na utekelezaji huo unaanza mwezi huu. Na Samuel Mwanga _ Maswa

POLENI SANA AMCOs Shinyanga Mwenge_Dakama Maswa kwa Ajari ya moto Kuunguliwa kwa pamba, lakini hakikisheni wanchi mnawalipa kama tu walikuwa wana madai yao.

Nianze kwa kutoa pole kwa Chama cha kushirikiana wilaya ya Maswa mkoa wa simiyu Hasa  vingozi wa amcos Kata ya Dakama kijiji cha Shinyanga mwenge kwa  ajari ya moto Iliyotokea na kusababisha Ghara la  kuhifadhia Pamba kuungua na kusababisha Hasara kwa Amcos ya takribani tan 120000 zilizowaka moto aidha nitoe pole kwa wananchi wa Shinyanga kwa kupoteza rasilimali hii adimu katika maghara lakini Viongozi wa Amcos Shinyanga Mwenge walipeni wanchi kama mliwakopa na mkapima Pamba yao kisha mkaiifadhi kwa kusubiri fedha na ili mwalipe,  kuungua moto maghara yenu ni sawa na ajari zingine lakini mkulima asihusike na Hasara hii kwani yeye   aliihifadhi vyema na akauza kwenu sasa hii ni  yenu viongozi wa AMCOS. Hatuhitaji kusikia wanchi hawajalipwa eti kwa kisingizi cha moto, moto ni  ajari kwenu na Hasara yenu kama Chama cha ushirika. Aidha niwaombe wanchi na vijana wenzetu muwe watulivu na wavumulivu na kuyafuata Yale viongozi wa cham cha ushirika na ser...