Posts

ASANTENI WAJUMBE WA MKUTANO MKUU WA CCM WILAYA YA MASWA

Mmenipa dhamana Ambayo kwangu naiona ni Bahati nzuri nitaitenda kama mlivyonituma Nitalipa wema Kwa wote  *Hodi mkoani tena

MUDA WA KUHESABIWA UMEWADIA HIVI SASA

Ndugu wananchi wenzangu,  Muda umeshawadia wa serikali yako kupata taarifa ya idadi yenu katika nzengo yenu hakikisha umehesabiwa hii ni Mhimu kwako, nzengo yako na serikali yako JITOKEZE UHESABIWE.

KUHESABIWA NI KUISAIDIA SERIKALI YAKO Ili IKUFIKIE

Kila mmoja ajiandae Kwa kuhesabiwa kwa kutoa taarifa sahihi za kidemographia na uchumi ili Taifa letu lipange na kuwa na mpango sahihi wa utekelezaji sahihi wa maendeleo ya Taifa letu kwa kufuata mlinganyo sahihi wa idadi sahihi ya watu na mpangilio sahihi wa makazi yetu SERIKALI NI KAMA FAMILIA lazima ujue idadi na mahitaji sahihi Kwa Wana familia. Usiku wa kuamkia 23/08/2022 kuwa tayali kuhesabiwa Onyesha ushirikiano Kwa makarani wa sensa. MASAGA JOHN PAUL     Mwasiliwa wa kutokuwa na idadi kamili ya Wana nzengo katika Kijiji CHANGU  maendeleo tunayapata Kwa kukadiliwa idadi yetu Jitokeze uhesabiwe

Mti mwema. Wenye maajabu.

Basi kukapambazuka siku yenyewe na mvua ilikuwa Bado inanyesha hata hivyo ilikuwa mvua ya wastani japokuwa watu hawakukata tamaa kuelekea kunako shughuli zao za Kila siku. Wakati tunatoka Ndani ya nyumba nje yake kulikuwa na mti aina ya mkwaju nikashangaa kuona matunda yake yakiwa yamekomaa yamewiva vizuri lakini matunda menyewe yapo utupu yaani yamemenywa ingali Bado yapo mtini na Kwa sababu ya mvua na unyevu ukwaju ule ulikuwa ukinata, Cha ajabu nilipotaka kuchuma walau tunda mojawapo ndipo macho yangu yakakutana uso Kwa uso na joka kubwa aina ya chatu, Ambapo kwenye huo mti lipo pango joka Hilo linaishi. Joka Hilo kubwa likaanza kutuvizia kuja upande tuliokuwa  kutaka kutumeza hata hivyo mawe yaliyokuwa chini, ng'hambo kidogo tuliyatumia kuliponda na baadae likawa limerudi Ndani ya pango lake kwenye utando wa mti huo wa mkwaju. Nikamwambia rafiki yangu mti huu hupondwa si Kwa sababu ya matunda Ila hupondwa Kwa sababu joka hili  juu ya mti, katikati linaziba au kuzuia ridhiki ya ...

KHERI YA MWAKA MPYA

Kwaniaba ya Umoja wa vijana wa chama Cha mapinduzi Wilaya ya Maswa, napenda kuwatakia Kheri ya mwaka mpya 2022. Ukawe mwaka wenye Kheri ,neema na Mafanikio makubwa kwa kila mmoja wetu. Masaga John Paul. Mwenyekiti wa UVCCM wilaya ya Maswa (M/k/ siasa)

SAMIA TENA 2025-30

Kwa Niaba ya vijana wote Kanda ya ziwa na  Kati bila ya kujari itikadi zetu za Dini ,siasa, ukanda au vyama vyetu vya siasa. Tunakupongeza kwa kuendeleza vyema taifa letu Tanzania kwa kudumisha Amani, Mshikamano na ustawi wa jamii. Taifa linasonga mbele kisiasa, uchumi na hata kijamii. Hongera Mhe SAMIA SULUHU HASSAN Vijana tunakuelewa zaidi.

DAKIKA 45 ZA KIPINDI CHA KWANZA KWANU WATEULE

Image
  Ndugu watanzania wenzangu , mabibi na mabwana vijana kwa wazee, nianze kwa kumshukuru Mungu kwa uzima na afya njema kwetu sote lakini nitoe pole kwa wale wote ambao hali zenu sio nzuri kiafya pamoja na mambo mengine, hata hivyo kila lililo kheri nawatakieni. Nianze kwa kumpongeza Dr John Pombe Magufuli Rais wa awamu ya tano wa jamhuri ya muungano wa Tanzania  kwa mara nyingine kwa  kuaminiwa na watanzania wote kuendelea kuwaongoza kwa ushindi wa kishindo wa zaidi ya asilimia 81, wakiwa pamoja na mwana mama hodari kabisa Samia Hassan katika uchaguzi mkuu wa october 2020. lakini kwa kipekee nikipongeze chama cha mapinduzi CCM chini ya uongozi wa dr John Pombe Magufuli kwa kuendelea kuaminika na Umma wa Tanzania  hata hivyo pongezi ziende kwao viongozi wa CCM wa ngazi zote kwa kazi kubwa walizofanya katika kuhakikisha CCM inaendelea kushinda chaguzi ili kuunda serikali. niishukuru serikali ya awamu ya tano kwa kutekeleza vyema na kishindo ilani ya uchaguzi ya mwaka 20...