Posts

PASAKA NJEMA

Nawatakieni PASAKA NJEMA ndugu wakristo na wànanchi wote AMEFUFUKA KWELI KWELI  ALIVYOSEMA, NIKWELI! NI KWELI! NI KWELI! ALELUYA! ALELUYA! ALELUUUYAAA!! Governor:  MASAGA JOHN PAUL

ASANTENI WAJUMBE WA MKUTANO MKUU WA CCM WILAYA YA MASWA

Mmenipa dhamana Ambayo kwangu naiona ni Bahati nzuri nitaitenda kama mlivyonituma Nitalipa wema Kwa wote  *Hodi mkoani tena

MUDA WA KUHESABIWA UMEWADIA HIVI SASA

Ndugu wananchi wenzangu,  Muda umeshawadia wa serikali yako kupata taarifa ya idadi yenu katika nzengo yenu hakikisha umehesabiwa hii ni Mhimu kwako, nzengo yako na serikali yako JITOKEZE UHESABIWE.

KUHESABIWA NI KUISAIDIA SERIKALI YAKO Ili IKUFIKIE

Kila mmoja ajiandae Kwa kuhesabiwa kwa kutoa taarifa sahihi za kidemographia na uchumi ili Taifa letu lipange na kuwa na mpango sahihi wa utekelezaji sahihi wa maendeleo ya Taifa letu kwa kufuata mlinganyo sahihi wa idadi sahihi ya watu na mpangilio sahihi wa makazi yetu SERIKALI NI KAMA FAMILIA lazima ujue idadi na mahitaji sahihi Kwa Wana familia. Usiku wa kuamkia 23/08/2022 kuwa tayali kuhesabiwa Onyesha ushirikiano Kwa makarani wa sensa. MASAGA JOHN PAUL     Mwasiliwa wa kutokuwa na idadi kamili ya Wana nzengo katika Kijiji CHANGU  maendeleo tunayapata Kwa kukadiliwa idadi yetu Jitokeze uhesabiwe

Mti mwema. Wenye maajabu.

Basi kukapambazuka siku yenyewe na mvua ilikuwa Bado inanyesha hata hivyo ilikuwa mvua ya wastani japokuwa watu hawakukata tamaa kuelekea kunako shughuli zao za Kila siku. Wakati tunatoka Ndani ya nyumba nje yake kulikuwa na mti aina ya mkwaju nikashangaa kuona matunda yake yakiwa yamekomaa yamewiva vizuri lakini matunda menyewe yapo utupu yaani yamemenywa ingali Bado yapo mtini na Kwa sababu ya mvua na unyevu ukwaju ule ulikuwa ukinata, Cha ajabu nilipotaka kuchuma walau tunda mojawapo ndipo macho yangu yakakutana uso Kwa uso na joka kubwa aina ya chatu, Ambapo kwenye huo mti lipo pango joka Hilo linaishi. Joka Hilo kubwa likaanza kutuvizia kuja upande tuliokuwa  kutaka kutumeza hata hivyo mawe yaliyokuwa chini, ng'hambo kidogo tuliyatumia kuliponda na baadae likawa limerudi Ndani ya pango lake kwenye utando wa mti huo wa mkwaju. Nikamwambia rafiki yangu mti huu hupondwa si Kwa sababu ya matunda Ila hupondwa Kwa sababu joka hili  juu ya mti, katikati linaziba au kuzuia ridhiki ya ...

KHERI YA MWAKA MPYA

Kwaniaba ya Umoja wa vijana wa chama Cha mapinduzi Wilaya ya Maswa, napenda kuwatakia Kheri ya mwaka mpya 2022. Ukawe mwaka wenye Kheri ,neema na Mafanikio makubwa kwa kila mmoja wetu. Masaga John Paul. Mwenyekiti wa UVCCM wilaya ya Maswa (M/k/ siasa)

SAMIA TENA 2025-30

Kwa Niaba ya vijana wote Kanda ya ziwa na  Kati bila ya kujari itikadi zetu za Dini ,siasa, ukanda au vyama vyetu vya siasa. Tunakupongeza kwa kuendeleza vyema taifa letu Tanzania kwa kudumisha Amani, Mshikamano na ustawi wa jamii. Taifa linasonga mbele kisiasa, uchumi na hata kijamii. Hongera Mhe SAMIA SULUHU HASSAN Vijana tunakuelewa zaidi.

DAKIKA 45 ZA KIPINDI CHA KWANZA KWANU WATEULE

Image
  Ndugu watanzania wenzangu , mabibi na mabwana vijana kwa wazee, nianze kwa kumshukuru Mungu kwa uzima na afya njema kwetu sote lakini nitoe pole kwa wale wote ambao hali zenu sio nzuri kiafya pamoja na mambo mengine, hata hivyo kila lililo kheri nawatakieni. Nianze kwa kumpongeza Dr John Pombe Magufuli Rais wa awamu ya tano wa jamhuri ya muungano wa Tanzania  kwa mara nyingine kwa  kuaminiwa na watanzania wote kuendelea kuwaongoza kwa ushindi wa kishindo wa zaidi ya asilimia 81, wakiwa pamoja na mwana mama hodari kabisa Samia Hassan katika uchaguzi mkuu wa october 2020. lakini kwa kipekee nikipongeze chama cha mapinduzi CCM chini ya uongozi wa dr John Pombe Magufuli kwa kuendelea kuaminika na Umma wa Tanzania  hata hivyo pongezi ziende kwao viongozi wa CCM wa ngazi zote kwa kazi kubwa walizofanya katika kuhakikisha CCM inaendelea kushinda chaguzi ili kuunda serikali. niishukuru serikali ya awamu ya tano kwa kutekeleza vyema na kishindo ilani ya uchaguzi ya mwaka 20...

TUSICHUKULIE POA CORONA INAZUILIKA

Image
Ndugu wadau wanahabari, vijana wenzangu, wasomaji pamoja na wasikilizaji wetu Habari zenu Binafsi. Nianze kwa kuwakumbusha na kuwafahamisha kuwa bado Duniani kote wanahangaika, kuzuia na kupambana na ugonjwa huu wa Corona. hata hapa Tanzania tayari tumekuwa tukipokea Taarifa na hali ya udhihiti wa ugonjwa huu wa Corona hata hivyo Niwaombe muendelee kufuaata maelekezo ya serikali ya namna ya kujikinga pamoja na kuzitekeleza kwa vitendo tahadhari zinazotolewa kupitia wizara ya afya na kamati iliyoundwa na waziri mkuu. Ndugu wadau wa habari  na Wana maswa mnaotumia mitandao kazaa ya kijamii whatsp, Instagram, Facebook na mingineneo zitumieni mitandao hizo kwa kuendele kuelimisha na kuikumbusha jamii na pia kuhamasisha usafi na uchukuaji wa tahadhari zinazotolewa na serikali kwani mitandao ya kijamii imekuwa ni chachu ya kupokea na kutoa Taarifa zinazojili tumieni muda wenu wa kukaa katika Magroup hayo kwa faida na kushusha hamasa hizo kwa familia zetu na jamii zetu zinazotuzunhuka. Ug...

MJUE BIBI TITI MWANAMKE SHUJAA NA HODARI MWENYE HISTORIA YA KPKEE TANZANIA

+255 🇹🇿🇹🇿🇹🇿 BIBI TITI MOHAMED: MWANAMAMA SHUPAVU NA MPIGANIA UHURU HODARI ALIYETINGISHA NA KUHESHIMIKA AFRIKA MASHARIKI NZIMA!!! 1. Usuli: 1.1 TITI Kuzaliwa: TITI MOHAMED SALUM MANDWAGA alizaliwa mwezi Juni 1926 jijini Dsm. 1.2 Wazazi Wa TITI: Baba yake aliitwa Bw. MOHAMED BIN SALIM na mama yake aliitwa Bi. HADIJA BINTI SALIM. Wazazi hawa walitokea Rufiji. Baba yake alikuwa mfanyabiashara ya mbuzi na ng'ombe na mama yake alikuwa mkulima. 2. Elimu: 2.1 Baba Agoma TITI Asisome: Baba yake alikataa katukatu kwamba TITI asisome shule kwa hofu angekuwa kafiri. 2.2 Mama Ampeleka TITI Shule: Baba yake alifariki TITI akiwa na miaka 9 tu. Mamaye akatumia fursa hiyo kumpeleka TITI Shule ya Wasichana Uhuru ambako alisoma hadi darasa la 4. 3. TITI Aolewa na MHENGA akiwa na miaka 14 tu: TITI aliolewa na mwanaume mzee ambaye angeweza hata kuwa baba yake wakati yeye akiwa binti wa miaka 14 tu. 4. TITI Ajifungua M...

ZIARA YA KATIBU MKUU WA CCM MASWA MKOANI SIMIYU YALETA NEEMA UKAMILISHWAJI WA JENGO LA KITEGA UCHUMI LA CCM. NYONGO ASHITUKIZA HARAMBEE

Image
Ziara ya katibu mkuu wa  chama cha mapinduzi CCM Taifa  Dr Bashiru Ally mkoani Simiyu Imetamatika katika wilaya ya Maswa ambapo pamoja na Mambo mengine Dr. Bashiru Ally aliweza kusimika Jiwe la  Msingi la  ujenzi wa  jengo la  kitega uchumi. na kuwahutubia mamia ya wanachama wa  CCM waliojitokeza kwa wingi kumraki na kumsikiliza katibu mkuu wa   CCM . katika hatua nyingine Mbunge wa Maswa  Mashariki na Naibu waziri wa  Madini Mheshimiwa Stanslaus . H. Nyongo alipopata wasaa wa  kusalimia aliweza kuhamasisha Harambee ya Papo kwa hapo   ili kukamilisha baazi ya mahitaji ya Jengo hilo Ambapo Mheshimiwa nyongo akiwa kama katibu wa  wabunge wa mkoa wa  simiyu aliwaita wabunge wote   waliokuwepo na akawaomba wamchangie chochote kwaajili ya ukamilishaji waa jengo hilo . Mhe   Nyongo alitoa mifuko 100 ya cement, na wabunge wote   walichangia Bati 150  wak...

KUTOKA UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA MWALIMU JULIUS NYERERE DAR.

Image
YALIYOJIRI WAKATI WA MAPOKEZI YA NDEGE MPYA YA AIRBUS 220-300 KATIKA UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA WA JULIUS NYERERE LEO TAREHE 23 DESEMBA, 2018 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli #Nawapongeza watanzania kwa kuamua kulipa kodi, tunafanya haya kwa sababu ya kulipa kodi, hongereni sana Watanzania. #Watanzania nawasisitiza tuwe wazalendo, hii ni kwa faida ya taifa letu. #Uchumi wa nchi yetu unaenda vizuri, tutunze amani yetu, tunarasilimali nyingi, Tanzania ni tajiri. #Pamoja na kuleta ndege mpya tunafufua karakana yetu kubwa ya matengenezo ya ndege iliyopo Kilimanjaro. #Tuliahidi kuimarisha huduma za usafiri, na katika miaka hii mitatu tumetekeleza ahadi hii kwa vitendo ikiwa ni kwa kufanya mambo makubwa ardhini, angani na hata majini. #Tunafanya upanuzi na ukarabati wa viwanja vya ndege 11 nchini, lengo ni kuendelea kuboresha sekta ya usafiri  wa anga. #Watendaji wakuu wa Serikali waliolipiwa tiketi za ndege za ATCL na hawakusafiri warudishe fedh...

MWANAMALUNDI, MSUKUMA ALIYEMSHINDA MKOLONI

Image
Kwa Hisani ya Mwandishi wa  kitabu chake NG'WANAMALUNDI SHUJAA WA WAKISUKUMA ALIYEWATESA WAJERUMANI. Kwa wale waliopata kusoma historia au kusikia hadithi za makabila, hasa ya Wasukuma na Wanyamwezi, hawakukosa kusikia habari ya Ng’wanamalundi. Mtu huyo aliyewahi kuutingisha utawala wa Wajerumani, alizaliwa katika ukoo wa kawaida akiwa mcheza ngoma mashuhuri, mwaka wa kuzaliwa kwake haufahamiki ila alifariki dunia mwaka 1936, akiwa tayari mtu mzima. Watu wengi wamekuwa wakimjadili kwa maoni tofauti, wengine wakimsifu kama shujaa huku wengine wakihusisha uwezo wake na nguvu za giza. Katika makala hii usahihi wa historia yake unaelezwa na mjukuu wake wa pili, Kishosha Sitta (80) mkazi wa Kijiji cha Mwalugulu wilayani Kahama mkoani Shinyanga, anayesimulia alivyomfahamu babu yake huyo. Sitta anaanza kueleza kuwa jina halisi la babu yake halikuwa Ng’wanamalundi bali lilikuwa Igulu Bugomola, ambaye alizaliwa katika Kijiji cha Mwakubunga Nera wilayani Kwimba mkoani Mwa...

Mwaka mmoja wa Mwenyekiti wa UVCCM (w) maswa.

Image
Ni mwaka mmoja sasa tangu uchaguzi wa Chama NA jumuia Ngazi ya wilaya NA kukamilika kwa safu ya uongozi kwa ngazi ya wilaya NA jumuia zake, Naam nilipata dhamana kubwa ya kuiongoza jumuia ya Vijana wenzangu kwa ngazi ya wilaya nikipata heshima ya kuwa Mwenyekiti uchaguzi uliokuwa wa Uhuru NA haki. Jumuia ya Vijana ni jumuia ambayo imebeba Leo yao NA kesho yao kwa vijana tunajitahidi sana kuyasemea mahitaji yao. NA pia kuzitatua changamoto zao kazaa, ikiwemo Ajira, Elimu, ujasiriamali, Mikopo vyuo na vyuo vikuu uwezeshwaji wa vijana hasa kupitia miradi yao kama MBOs, NGs, na hasa uwezeshwaji wao wa mikopo nafuu Kutoka halmashauri yetu ya Maswa. Lakini katika kipindi hiki cha mwaka mmoja tumeendelea kuwafikia vijana wenzetu hasa kupitia ziara ambapo tunapata nafasi ya kuwasikiliza kuwashauri na kuwajengea uwezo na kuwapa Hamasa ya kuyakabiri MAISHA ndani ya Chama na MAISHA ya kawaida nje ya Chama ( we are  empowering them and sensitizes, for their self awareness) ili kupata vijana s...

KUELEKEA MTIHANI WA TAIFA MWEZI MEI, WANAFUNZI 1003 KIDATO CHA SITA SIMIYU WAPIGA KAMBI YA KITAALUMA

Na Stella Kalinga Simiyu Takribani wanafunzi 1003 wa Kidato cha sita kutoka shule za Sekondri 11 zenye kidato cha tano na sita Mkoani Simiyu wamepiga kambi katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa na Shule ya Sekondari Binza, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya Mtihani wa Taifa ambao unatarajia kufanyika mapema mwezi Mei mwaka huu. Akifungua kambi hiyo leo  katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa wilayani Maswa, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Anthony Mtaka amesema ili mkoa huo uweze kushindana na kufanya mageuzi katika Uchumi ni lazima kuwekeza katika elimu. “Kama wanafunzi wetu wanakaa makambi ya michezo ngazi ya kata, wilaya, mkoa na Taifa kwa nini wanafunzi hao hao wasikae  kambi kwa ajili ya maendeleo ya taaluma; tukitaka kufanya mageuzi ya Mkoa huu ni lazima tuweke nguvu kwenye elimu, maeneo yenye uchumi mzuri wamewekeza sana kwenye elimu” alisema Mtaka. Aidha, Mtaka awataka wanafunzi wote wa kidato cha sita kuwasikiliza walimu watakaokuwa wakiwafu...

TUUNGE MKONO JUHUDI ZA VIONGOZI WETU TUIJENGE MASWA YETU

Image
      MASWA YETU          Anaandika mothes mbembela Ndugu wapenzi wasomaji wa Makala zangu Napenda kuwaalika tena katika uchambuzi wa makala zangu ambazo mara nyingi zimekuwa zikiegemea katika kujadili masuala mbalimbali kutoka katika wilaya yangu ya Maswa mkoani Simiyu. Leo katika makala hii ningependa kujikita zaidi katika kutabainisha mambo mbalimbali ya kijamii, kiuchumi na kisiasa ambayo kwa kiasi kikubwa yanafanya MASWA YETU ionekane angavu Daima. Katika wilaya yetu Maswa Juhudi mbalimbali zimeweza kufanywa na viongozi kwa kushirikiana na wananchi wao kuhakikisha kuwa wilaya yetu haipo mbali ktk kilele cha maendeleo, kwa ufupi tu niweze kuorodhesha mambo na assets mbalimbali ambazo kwa Hakika Maswa Tunajivunia. 1. Tuna Hospitali kubwa ya wilaya ambayo imekuwa ikihudumia maelfu ya wagonjwa kutoka sehem mbalimbali za nchi yetu tena kwa kiwango cha juu kabisa (Science and Technology) Hongera ya pekee imfikie Dokta...

TUONGEZE JUHUDI KUFANYA KAZI NA KUMPA USHIRIKIANO RAIS WETU

Image
Nianze kwa kuwapa pole na majukumu mazito kwenu viongozi na watanzania wote popote mlipo kwa kazi na majukum makubwa ya kila siku mnayofanya, hii yote ni katika kuutengeneza mkate wa kila siku na wajibu wako kama sehemu ya kuijenga Tanzania mpya na familia zetu. Sambamba na pole hii niwapongeze kwa kazi nzuri mnazozifanya kuhakikisha tanzania yetu inasonga mbele (SISI NI TANZANIA MPYA). hakuna asiyejua kuwa zama hizi ni zama za kazi na hasa kazi ya kuijenga Tanzania mpya Tanzania ya uchumi wa kati na ya viwanda naomba kusema yafuatayo. ndugu watanzaia wenzangu Tanzania mpya ni Tanzania ambayo watu wake wanapaswa kuwa wazalendo  katika kutimiza majuku yetu ya kila siku kwa nafasi zetu tofauti tofauti ni wajibu wetu kufanya kazi kizalendo ili kutimiza wajibu wetu vizuri wa kuijenga Tanzania mya.  Tanzania tunayo bahati kubwa kuwa miongoni mwa taifa ambalo Rais wake ni Mzalendo anayelipenda taifa lake kwa moyo wake wote na nguvu zake zote zote, anfanya kazi kubwa yeye pa...

UVCCM MASWA, YATOA PONGEZI MALUUMU KWA VIONGOZI WA MKOA WA SIMIYU